Παρασκευή 30 Οκτωβρίου 2015

AFRIKA MAGHARIBI: Hatua za Pamoja Dhidi ya Uharamia



Noël Kokou Tadégnon  

Tayari kuna zaidi ya mashambulizi matatu ya meli yaliyofanywa na maharamia katika Pwani ya Afrika Magharibi mwaka huu. Serikali za kikanda zitakutana mjini Cotonou, Benin mwezi Oktoba kujadili jitihada za pamoja za kutokomeza uharamia.

LOME, Oct 10 (IPS) -
Takwimu za mashambulizi zinatokana na matukio yaliyoripotiwa na waongoza meli kwa Kituo cha Kimataifa cha Kutoa Taarifa za Uharamia Baharini na zinaonyesha tishio linalozidi kuongezeka la usafiri wa meli katika ukanda wenye utajiri wa mafuta.

Mashambulizi ya karibuni zaidi ni yale ya Sep. 15 dhidi ya meli ya mafuta ya Mattheos I ikiwa na wafanyakazi wake 23 katika pwani ya Togo. Siku kumi baadaye, wamiliki wa meli kutoka Hispania waliviambia vyombo vya habari kuwa meli hiyo na wafanyakazi wake wameshaachiliwa huru; bila kulipwa kwa fedha zozote zile zilizodaiwa na watekaji lakini baadhi ya mafuta ya dizeli yaliibwa katika meli hiyo.

Serikali katika mwambao wa Afrika Magharibi zimeonyesha wasiwasi wao kuhusu kuongezeka kwa idadi ya mashambulizi dhidi ya meli za mizigo, na zinataka kukusanya rasilimali chache walizonazo kuendesha hatua za pamoja, kama vile kushika doria katika Ghuba ya Guinea.

"Lakini hatutaki kuishia tu kwenye doria za pamoja kati ya Benin na Nigeria; hivi karibuni tutaenea na kuhusisha majeshi ya Togo na Ghana," Kamanda Maxime Ahoyo, mkuu wa Jeshi la Majini la Benin, aliiambia IPS.

"Kama tutakabiliana na matatizo ya uharamia katika maji ya Benin lakini, kwa mfano, tutaacha kuchukua tahadhari za kiusalama katika maji ya Togo, na kama hatutaungana na wenzetu wa Togo na nchi nyingine, hali hii – ambayo ina mtandao mpana – itazidi kuenea."

Madhara ya kiuchumi

Rais wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Mataifa ya Afrika Magharibi, James Victor Gbeho, ametoa wito wa kuchukuliwa kwa hatua dhidi ya uharamia na kupanuliwa na kuingiza mataifa yote katika pwani.

"Majeshi ya majini katika mataifa yetu yote ya ukanda wa pwani yanapaswa kuunganisha nguvu zao siku zote," Gbeho aliiambia IPS, huku akisitiza imani yake kuwa tatizo la uharamia lazima kupatiwa ufumbuzi kamilifu. "Hali hiyo inazidi kutisha na inaweza kuwa na madhara makubwa ya kiuchumi kwa nchi zetu. Hii ndiyo sababu tutachukua hatua dhidi yake."

Uharamia tayari umeshasababisha makampuni ya bima ya vyombo vya baharini mjini London kuiingiza Benin katika orodha ya kuwepo katika ukanda wa hatari kubwa ya usafiri wa meli. Makampuni ya bima ya vyombo vya baharini yanayowakilishwa na chama cha ‘Lloyd's Market Association’ yanadai ada kubwa kulipia meli zinazopita katika ukanda huo.

Kulingana na Bénetti Gagalo, Katibu Mkuu Msaidizi wa Chama cha Walaji cha Togo, hali hiyo ni wazi itakuwa na madhara katika kipato cha bandari za ukanda huo ikiwa ni pamoja na gharama za bidhaa za walaji.

Msaada kutoka nje

Dharula ya hali hiyo imesababisha serikali za kikanda kuomba msaada kutoka Ufaransa na Marekani, ambao wameshapeleka vifaa vya majini katika eneo hilo.

Manuwari ya Kifaransa ya Germinal, tayari inafanya doria katika pwani ya Benin, Togo na Ghana kujaribu na kupunguza uharamia, ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo kwa askari wa majini kutoka nchi zote tatu.

"Tumewapatia mafunzo askari hawa wa majini, na wameshiriki katika mazoezi yote ya kiusalama na kufanya doria ambayo tumeyafanya kuzuia uharamia. Na wametusaidia na maarifa yao waliyonayo katika eneo hili la oparesheni," Sébastien Chatelin, nahodha wa manuwari hiyo ya Kifaransa, aliiambia IPS.

Manuwari ya Kimarekani, HSV Swift, pia imefika katika Ghuba ya Guinea, ikisaidia kupambana na uharamaia huku ikitoa mafunzo kwa askari wa majini wa Benin, Togo na Ghana kama sehemu ya mpango wa kijeshi wa Marekani ujulikanao kama "Africa Partnership Station".

"Lengo letu ni kujaribu na kutoa mafunzo kwa washirika wa Afrika juu ya usalama," alisema nahodha wa chombo hicho cha Marekani, Rhett S. Mann.

"Mpango wa APS utaturuhusu kufanya kazi pamoja kukabiliana na matatizo ambayo yanaathiri maji ya pwani yetu," aliongeza Sam Nkruma, ofisa kutoka jeshi la majini la Ghana.

Askari mwenzake wa Benin, Christian Oussa, alikaribisha mafunzo waliyopata wakiwa katika meli mbili za jeshi la majini. "Hii itaturuhusu kukabiliana na uharamia na wafanyabiashara haramu katika bahari. Tumejifunza jinsi ya kupanda meli zinazotiliwa mashaka na kuzikagua; mafunzo ni mazuri mno," aliiambia IPS. (END/2011)


‘Nchi za Afrika ziungane kudhibiti uharamia’

Ili kukabiliana na vitendo vya uharamia kwenye wa Bahari ya Hindi, nchi za Afrika zimetakiwa

Mwananchi


Dar es Salaam. Ili kukabiliana na vitendo vya uharamia kwenye wa Bahari ya Hindi, nchi za Afrika zimetakiwa kuweka nguvu katika ushirikiano, kwa kuwa si rahisi nchi moja kudhitibi uhalifu huo unaofanya na watu wanaodaiwa kuwa ni raia wa Somalia.
Hayo yalisemwa jana na mkurugenzi wa Mashtaka Tanzania (DPP), Biswalo Mganga wakati akifungua mkutano wa waendesha mashtaka na wapelelezi wa kesi za uharamia kwa nchi zilizopo ukanda wa Afrika Mashariki.
Alisema kuna baadhi ya meli zinakwepa kupita pwani ya Somalia kwa hofu ya maharamia na kulazimika kuzunguka umbali mrefu.
“Matokeo yake, bei za bidhaa zinazoingizwa na meli hizo zinakuwa juu kutokana na kufidia gharama za usafirishaji zinazotokana na meli kutumia njia ndefu,” alisema Mganga.

DPP alisema meli zinazopita pwani ya Somalia zimekuwa zikitozwa kiasi kikubwa cha bima na kwamba gharama hizo zimekuwa zikifidiwa na watumiaji wa bidhaa zinazoletwa na meli hizo.
“Wakati maharamia wanaungana kufanya uhalifu, nasi kama mataifa tunaoathirika na matukio haya tunatakiwa kuungana ili kupambana nao,” alisema.
Aliwataka waendesha mashtaka na wapelelezi wa masuala ya uharamia kubadilishana uzoefu na mbinu za kushughulikia wahalifu hao ili waweze kuadhibiwa.

Naye, balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini, Filiberto Sebregondi alisema umoja huo umekuwa ukitoa rasilimali fedha kwa ajili ya kupambana na uharamia kwenye Bahari ya Hindi.
“Tunataka waendesha mashtaka wa makosa ya uharamia katika nchi zilizoko katika pwani ya Bahari ya Hindi, kubadilishana uzoefu kwa lengo la kuwadhibiti maharamia hawa,” alisema.
Sebregondi alisema maharamia hawana mipaka na kwamba nchi mbalimbali zinatakiwa kuweka mtandao wa ushirikiano ili kuwakamata.
“Ni jambo muhimu kwa nchi husika kuliangalia kwa ukubwa zaidi suala hili, kwa kuwa kinyume chake ni kuruhusu uharamia kuendelea,” alisema.
Mkutano huo unashirikisha waendesha mashtaka kutoka nchi za Tanzania, Somalia, Djibouti Shelisheli, Mauritius, Yemen na Kenya.

Ona pia

Uharamia Afrika Magharibi

Uharamia biashara katika Pembe ya Afrika (2008)

'Kipindupindu chaweza kuenea hadi nje ya Tanzania'


Iran Swahili Radio

'Kipindupindu chaweza kuenea hadi nje ya Tanzania'Shirika la Afya Duniani (WHO) limeionya Tanzania juu ya kuenea ugonjwa hatari wa kipindupindu nchini humo na kwamba ikiwa hatua za maana hazitochukuliwa, basi kuna uwezekano ugonjwa huo ukaenea hadi nchi jirani pia. Dominique Legros, mkuu wa kitengo cha kupambana na maambukizi ya ugonjwa wa kipindupindu cha shirika hilo amesema kuwa, hadi sasa kuna kesi 5000 za maambukizi ya ugonjwa huo nchini Tanzania.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, tangu mwezi Agosti mwaka huu hadi juzi tarehe 21 Oktoba, jumla ya kesi 4,922 za maambukizi ya kipindupindu zilikuwa tayari zimeripotiwa. Dominique Legros ameitaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua za haraka za kuzuia kuenea ugonjwa huo nchini Tanzania, ili kuzuia pia maambukizi hayo katika nchi jirani. Aidha mkuu huyo wa kitengo cha WHO cha kupambana na ugonjwa wa kipindupindu amesema kuwa, kukosekana maji salama ya kunywa, ndiyo sababu kuu ya kuenea kwa kasi ugonjwa wa kipindupindu nchini Tanzania. 
Mara ya mwisho kuenea ugonjwa wa kipindupindu katika eneo la Afrika Mashariki ilikuwa mwaka 1990, ambapo katika kipindi hicho karibu watu laki mbili waliambukizwa ugonjwa huo ndani ya nchi nne wanachama wa EAC, huku karibu watu wengine 8000 wakipoteza maisha.

Ulaji wa nyama za binadamu na jinai nyingine S/Kusini


Iran Swahili Radio

 Ulaji wa nyama za binadamu na jinai nyingine S/Kusini Ripoti iliyotolewa hivi karibuni imefichua kuwepo vitendo vya kuwalazimisha watu kula nyama au viungo vya ndani ya miili ya wanadamu wenzao, kunywa damu, ubakaji na vitendo vingine vya ukatili kutoka pande zote mbili zinazohusika katika mzozo  huko Sudan Kusini.
Ripoti hiyo ni matokeo ya uchunguzi uliofanywa na Kamisheni ya Uchunguzi ya Umoja wa Afrika kuhusu Sudan Kusini. Ripoti hiyo imeituhumu serikali na waasi wa Sudan Kusini kuwa wamefanya ukatili na unyanyasaji mkubwa kwa raia wa nchi hiyo. Ripoti hiyo yenye kurasa 342 imeongeza kuwa, kuna ushahidi wa kutosha kwamba mauaji, vitendo vya ubakaji, utumwa wa ngono, mateso na aina nyingine za ukiukaji wa haki za binadamu vimefanywa na pande mbili husika kwenye mzozo wa Sudan Kusini. Madai ya kutolewa damu kutoka katika miili ya watu mara baada ya kuuliwa na kuwalazimisha wengine kutoka kabila mojawapo la jamii ya nchi hiyo kunywa damu au kula nyama zilizochomwa za miili ya wanadamu wenzao, ni miongoni mwa jinai zilizoorodheshwa katika ripoti hiyo ya AU.

Ona pia

«I lit the charcoal briquettes at the one end of a magazine of bullets from a kalashnikov, placed the incense on top of them and censed the people accompanying me» (Experiences from South Sudan)

Πέμπτη 29 Οκτωβρίου 2015

Uharamia Afrika Magharibi

dw.com

Tunapozungumza kuhusu uharamia barani Afrika hii leo, fikra ya kila mmoja huelekea Somalia. 

Cotonou, mji mkuu wa Benin

Lakini pwani ya Afrika magharibi imegeuka kuwa eneo la pili hatari kwa maharamia wanaolenga hususan mafuta na meli za kemikali wakitumia silaha za kutegeshwa na miripuko ya roketi.´
Uharamia katika pwani ya Afrika magharibi unaongezeka katika kiwango cha kushtusha na unatatiza vibaya mpangilio wa biashara ya kimataifa. Pwani ya Afrika magharibi imeshuhudia zaidi ya mashambulio 20 dhidi ya meli za kemikali na za mafuta katika nusu ya kwanza ya mwaka huu [2011].
Nchi ya Benin peke yake imeripoti visa 15. Vyombo sita vya baharini vimetekwa nyara. Maharamia waliwalazimisha manahodha wa meli kuzielekeza meli zao katika maeneo yasiyojulikana, ambapo mizigo kwenye meli hizo yaliibiwa, huku mabaharia kadhaa wakijeruhiwa.

Bandari ya Cotonou, Benin

Maxime Ahoyo ni kamanda wa jeshi la majini la Benin. Anasema serikali nyingi katika eneo hilo zina wasiwasi mkubwa kuhusu mashambulio hayo. Na ndiyo sababu serikali ya Benin imeamua kuliongeza nguvu jeshi lake la majini.
' Tunatarajia ndege mbili za kijeshi zilizo na kamera za kuweza kuona usiku. Ndege hizo ndogo zinapangwa kuwasilishwa mwezi Septemba kutoka Ufaransa. Na Boti tatu za kupiga doria zinatengenezwa Ufaransa. Zitawasili mwezi Februari mwaka 2012'.
Ahoyo anaeleza kuwa punde tu boti hizo zitakapowasili mwezi huu, Benin itaimarisha usalama katika bahari yake. Boti hizo zitaweza kusafiri kwa umbali mkubwa na zitaweza kusafiri haraka katika bahari kubwa ambapo maharamia huzitegesha meli zao ili kuweza kuiba mizigo.
Pottengal Mukundan ni mkurugenzi wa ofisi ya kimataifa ya ubaharia nchini Uingereza na anaeleza kuwa njia ambazo meli zinatekwa nyara Afrika magharibi ni sawa na kama ilivyo Afrika mashariki.
'Wanatumia mbinu sawa za mashambulio, wanajitokeza kwenye viboti vidogo, na silaha za kutegeshwa na miripuko ya roketi na huzilazimisha meli kupunguza kasi au kusimama, na baada ya hapo wanapanda kwenye meli hizo'.
Hata hivyo maharamia katika Afrika ya magharibi, wana malengo tofauti na wenzao wa Somalia. Maharamia wa Somalia huziteka meli na mabaharia waliomo kwenye meli hizo, na baadaye wakadai malipo ya fedha ili wawaachilie. Kwa upande wa maharamia wa Afrika magharibi, maharamia hao huiba mizigo iliyomo kwenye meli hizo, nayo huwa ni mafuta na mitungi ya gesi ambayo huyauza katika soko haramu. Bamidele. A. Ojo, ni mtaalamu wa masuala ya kigaidi katika chuo kikuu cha Dickinson nchini Marekani.
'Unapokuwa na shughuli za kihalifu ambazo zinaathiri usafirishaji mafuta, ina maana kuwa ni lazima uzidishe usalama katika meli, ni lazima uongeze hatua za kiusalama kuziongoza meli hizo wakati zinaposafirisha mafuta ghafi kutoka Afrika magharibi hadi Ulaya, na hilo bila shaka litaongeza thamani ya mafuta na bei itaweza kuwasilishwa kwa watu binafsi katika eneo la Ulaya ya magharibi na Marekani'.
Hata hivyo vyombo vya habari vya kimataifa havijaangazia ongezeko la visa vya uharamia katika pwani hiyo ya Afrika magharibi. Serikali za Afrika magharibi zinafikiria kuwa mpango wa pamoja ni suluhu iliyo bora kukabiliana na mashambulio ya maharamia.
Hata hivyo wataalamu wanasema inahitaji jitihada zaidi, kuliko ununuzi wa boti mpya za kupiga doria kwa jeshi la majini katika eneo hilo. Na wanasema huenda mfumo huo wa pamoja wa ulinzi usiwepo hivi karibuni kwa kuwa nchi katika eneo hilo ni maskini mno kuweza kuugharamia.

Mwandishi: Alice Kiingi/ Maryam Abdalla
Mhariri:Josephat Charo

Ona pia

Important speech of the Patriarch of Alexandria and All Africa Theodoros II, in the Pan-African Parliament


Patriarchate of Alexandria

05/10/2015

Your Excellency Mr. Roger Nkodo Dang, President of the Pan-African Parliament,
Your Excellencies Ladies and Gentlemen Parliamentarians of the African Continent,

I am here among you today following a kind invitation from our President, who comes from the beautiful country of Cameroon where I served in the past as Metropolitan, having Yaoundé as the Centre of my Ministry to the West African Countries.

As Primate of Orthodoxy in Africa I strive to provide a podium and voice to our suffering African brothers and sisters, especially the poor and orphaned children, who look to all of us through our common actions so that they too can live happily and look to the future with hope.

I am here today, in the temple of African Democracy, to convey to one of the most important African organization, the Pan-African Parliament, our present common anxieties, as well as our common hopes for the future of the poor and orphaned children of Africa, as well as our suffering brothers and sisters, who in spite of times and circumstances, remain faithful to the sacred institution of family, so that all of us on the African Continent can experience a better future in social progress, prosperity, security and peaceful coexistence and cooperation.

In our contemporary world unfortunately we are again experiencing in our everyday life the distressing results of religious fundamentalism. Our fellow humans are murdered or forced to leave their homelands and become refugees in search of a safe place for their children to live in, all because of their different religious beliefs. There is no doubt that behind every religious conflict there are hidden political conflicts and interests, as well as attempts at geopolitical reclassifications which do not take into account human lives.

However, you and we, in other words the political leaders and we the religious leaders, bear an ENORMOUS responsibility for the peaceful progress of our Continent and our world at large. It is on your political decisions, of coexistence and peace, that we must both structure our individual and common activities for reconciliation and mutual understanding, so that we can both plan for the future of our children outside of and beyond poverty and war; destruction and fear. 

Our Patriarchate, the Throne of the Apostle Mark, never once throughout its twenty centuries of existence, sheltered, supported, or promoted religious conflicts. Religious differences, like political ones, are solved through dialogue and mutual understanding. Our Patriarchate comes into contact with and exchanges points of view with other religious entities, while participates actively in all Christian dialogue with the other prominent monotheistic religions, namely Islam and Judaism.

As Pope and Patriarch of Alexandria, in awe and in fear of God, I try to the best of my abilities, to be helpful to the people of Africa, the ordinary people of toil, of disease and illiteracy, so that I can contribute as much as possible to the eradication of poverty, oppression and the exploitation of man by man. 

My presence here once again places me in front of the responsibilities which we all have, as political or spiritual leaders of our Continent, to strive even more vigorously to limit and eradicate these phenomena. We have to work and live together on this Continent in an environment of peace and progress. I therefore welcome with sincere joy and satisfaction, your cooperation with the Inter-Parliamentary Assembly for Orthodoxy. It is a political organization which has been highly regarded in the political realms worldwide for the past twenty-three years and through every means available it fights against poverty and destitution, for peace and coexistence between people across borders, races and cultures. I am sure that your collaboration with the Inter-Parliamentary Assembly for Orthodoxy will be productive for our great wounded continent. It will lead you to further collaborations in other places, such as the European Parliament.

We have been informed that for the first time this year by decision taken by the Plenary Session of the European Parliament, following the elections of 2014, that a permanent standing interparty committee has been formed, for religious freedom and tolerance. We also learned with great satisfaction that the Inter-Parliamentary Assembly for Orthodoxy has substantially contributed to the creation of this Standing Committee and furthermore has close cooperation with it. I believe that we also should move on to something more permanent which will focus on the collaboration and tolerance between different religions and will exceed good intentions and wishes. 

Your Excellency, Ladies and Gentlemen Parliamentarians,
Based on your recent decisions and declarations, you firm intention is to evolve this body, the Pan-African Parliament, into a major strategic organization for the entire Continent, so that the problems of our people can emerge as problems of the Continent. 

You have decided to seek solutions on technical projects and infrastructure which concerns the entire Continent; to create the necessary tools, the necessary groups of experts, which will allow you to address problems and formulate solutions on a continental level thus providing a more holistic approach to problems that are common to our continent and to contribute to the establishment of rules of law which will be common for the whole of our Continent. 

New technologies, which offer nowadays ever greater possibilities, constitute an valuable ally for you. Your efforts fill us with satisfaction and we discern through them a better future for all of us. This invaluable effort of Pan-African political understanding and perspective, which your Parliament is establishing, in order to be complete and comprehensive, should take into account both the social and cultural-religious dimensions of the people of Africa. It is on such a noble political level that we must approach the dialogue between cultures and the cooperation of religious expression in Africa. 

Every effort that has to do with the future of Africa, must have as its starting point and its reference, the cultural mutual understanding and cooperation of nations and people. The future of Africa, its prospects, is ultimately based on the possibility which we must develop, so that we can ensure principles and structures of peaceful coexistence and understanding. 

Our Patriarchate and I personally as Pope and Patriarch of the Great City of Alexandria, are ready to contribute to such a plan, such a perspective, for a permanent place for religious dialogue between the cultures within the framework of your parliament and your cooperation with the Inter-Parliamentary Assembly for Orthodoxy.
God bless you all!

See also

THE PATRIARCH OF ALEXANDRIA GIVES THE KEYNOTE ADDRESS TO THE PAN-AFRICAN PARLIAMENT

Picha takatifu katika Kanisa la Orthodox


 

 Yesu katika ulimwengu wa wafu, pamoja na maiti kale (angalia hapa - kwa lugha ya Kiingereza)

Sw.wikipedia.org (na hapa)

Picha takatifu (kwa Kigiriki εἰκών, eikōn "picha"; ing. icon) kwa kawaida ni mchoro unaoheshimiwa kidini hasa katika Ukristo wa Mashariki lakini pia katika madhehebu mbalimbali ya Ukristo wa Magharibi, kama vile Kanisa la Kilatini.

Mara nyingi picha hizo zinamhusu Yesu, Bikira Maria, watakatifu wengine, malaika na msalaba.

"Sanaa ya Kikristo" inataja kwanza kati ya karne ya 2 na karne ya 3 katika maandishi ya Tertuliani (160 hivi - 220) na Klemens wa Aleksandria (150 hivi - 212).

Matumizi ya picha hizo yalipingwa na baadhi ya Wakristo, hasa wa mashariki, baada ya Uislamu kutokea na kuenea katika maeneo yao.

Hatimaye Mtaguso wa pili wa Nisea (787) ulithibitisha uhalali wa picha hizo na wa heshima ambazo zinapewa, kama ulivyotetewa hasa na mtakatifu Mwarabu Yohane wa Damasko.

 
Ngazi ya Kupanda kwa Mungu ni picha ya karne ya 12 
inayoonyesha wamonaki wakipanda kwa 
Yesu mbinguni, Monasteri ya Mt. Katerina, Sinai
 

Picha takatifu inayodokeza fumbo la Utatu kwa kuchora malaika 
watatu waliolakiwa na Abrahamu huko Mambre. 
Ilichorwa na mmonaki mtakatifu Andrej Rublëv (1360-1427) 
na kwa sasa inatunzwa Moscow, Tretjakow Gallery (hapa).

 
Picha ya Mt. Nikolasi iliyochongwa jiweni kati 
ya karne ya 12 na karne ya 15, Radomysl Castle, Ukraine

Mtaguso wa pili wa Nisea 



Roho Mtakatifu akionekana Kama Njiwa, katika Ubatizo wa Kristo (hapa)

Mtaguso wa pili wa Nisea uliitishwa na malkia Irene wa Bizanti mwaka 787, ili kujadili matumizi ya sanamu katika Ukristo, kutokana na ombi la [Orthodox] Papa Adrian I (772-795).

Wakristo wengi wanauhesabu kuwa wa saba kati ya Mitaguso ya kiekumeni. Ni wa mwisho kufanyika wakati wa mababu wa Kanisa.

Mtaguso mkuu huo ulihitajika ili kumaliza mabishano makali kuhusu sanamu za Kikristo yaliyochukua zaidi ya miaka 100 hasa katika Dola la Roma Mashariki yakimalizika mwaka 843 tu.

Chanzo ni uamuzi wa kaisari Leo III wa Bizanti (717-741) wa kuteketeza sanamu zote ili kujilinganisha na Waislamu waliotishia utawala wake.

Patriarki wa Konstantinopoli alilazimika kujiuzulu, lakini uamuzi wa kaisari ulizidi kupingwa hasa na wamonaki na mwanateolojia Yohane wa Damasko. Mapapa wa Roma pia walipinga uamuzi huo. 


 

Yohane wa Damasko 
 
Sera ya dola ilibadilika aliposhika uongozi Irene kwa niaba ya mtoto wake mdogo Konstantino VI wa Bizanti.

Mtaguso ulianza Konstantinopoli mwaka 786, lakini ulipoingiliwa na jeshi waliowaunga mkono maaskofu wengi waliopinga sanamu, Irene aliuhamishia Nisea ambapo vilifanyika vikao 7 kuanzia tarehe 28 Septemba 787. Cha mwisho kilifanyika katika ikulu tarehe 23 Oktoba 787.

Pamoja na maaskofu 300 hivi wa dola hilo, walihudhuria wamonaki wengi. Papa alituma mabalozi wake wawili na barua moja.

Mtaguso ulitofautisha heshima inayokubalika kwa sanamu na ibada isiyovumilika. Hoja kuu ni kwamba sanamu si kitu, ila inamwakilisha yule aliyechorwa ndani yake. Kimsingi sanamu zinakubalika kutokana na umwilisho wa Mwana wa Mungu uliomfanya atwae sura na kuonekana.

Mtaguso ulichukua pia maamuzi mbalimbali ili kurekebisha Kanisa.


 
 
Elizabeti na Bikira Maria (hapa)

Tanbihi 
 
Bogomolets O. Radomysl Castle-Museum on the Royal Road Via Regia". — Kyiv, 2013 ISBN 978-617-7031-15-3
Marejeo
Beckwith, John, Early Christian and Byzantine Art, Penguin History of Art (now Yale), 2nd edn. 1979, ISBN 0-14-056033-5
Marejeo mengine
Evans, Helen C. (2004). Byzantium: faith and power (1261-1557). New York: The Metropolitan Museum of Art. ISBN 1-58839-113-2.
Evans, Helen C. & Wixom, William D (1997). The glory of Byzantium: art and culture of the Middle Byzantine era, A.D. 843-1261. New York: The Metropolitan Museum of Art. ISBN 978-0-8109-6507-2.


Mtatatifu Dimitrios (hapa)


Viungo vya nje 

Orthodox Iconography by Elias Damianakis
A Discourse in Iconography by St. John of Shanghai and San Francisco
The Iconic and Symbolic in Orthodox Iconography
Icon & worship - Icons of Karakallou Monastery, Mt.Athos
Contemporary Byzantine icon studio, iconography school and orthodox resources
Iconography Guide -free eLearning site
Orthodox iconography by Fr. Theodore Koufos
On the difference of Western Religious Art and Orthodox Iconography
Church of the Nativity - Explanation of Orthodox Christian Icons
Concerning the Veneration of Icons
Holy Icons: Theology in Color (Antiochian Orthodox Archdiocese)


Ona pia

Yesu Kristo - Mungu akawa mtu na mtu inakuwa kama mungu
Utatu Mtakatifu, Mungu ambaye anapenda ubinadamu
Kanisa la Orthodox na Kanisa Katoliki

Katika mwanga wa Mungu
Historia ya Kanisa la Orthodox : Ukristo barani Afrika
Ortodox Mkristo Liturujia takatifu katika Kasoa, Ghana
 


Bikira Maria, Mama wa Mungu
God the Holy Trinity: ‘The Lover of Mankind’ (& the "depiction of God" in Orthodox Church)
Historicals & miraculus orthodox holy icons of Theotokos (tag)
Historicals & miraculus orthodox icons of the Theotokos from all the World
Le rôle de la matière dans l'iconographie et les arts liturgiques

Τρίτη 27 Οκτωβρίου 2015

Le rôle de la matière dans l'iconographie et les arts liturgiques

 
"Ô Christ, que pouvons-nous t'offrir en présent * pour être apparu sur terre en notre humanité? * Chacune de tes créatures, en effet, * exprime son action de grâce en t'apportant:
*les Anges, leur chant,* le Ciel, une étoile, * les Mages, leurs cadeaux,* les Bergers, l'émerveillement, * la Terre, une grotte, * le Désert, une crèche * et nous-mêmes une Mère vierge. * Dieu d'avant les siècles, aie pitié de nous.. "[1]

La Déipare du Don
panneau Tempera à l'oeuf avec des pigments naturels
(comprenant des ocres de la forêt de Dean en Angleterre
et du lapis-lazuli d'Afghanistan) et or 24 carats , 2011
 

 Les arts liturgiques de la Sainte Eglise Orthodoxe servent à nous orienter vers la beauté ineffable du Royaume céleste de Dieu et sont une fenêtre ouverte sur elle, qui nous révèle la nouvelle Jérusalem et à travers ses saints mystères et l'iconographie nous met en communion avec le Christ, la Mère de Dieu et les grands saints de l'ancien et nouveau. Se trouver plongé dans cet environnement sacré est une expérience profonde qui se fait par le biais de tous les arts liturgiques qui travaillent ensemble dans une symphonie sacrée qui transporte notre être dans le royaume de l'éternel et de l’ineffable. 

 Les principes intemporels théologiques sur lesquels les arts liturgiques sont fondées, le respect et la compréhension de la langage sacré des formes et des couleurs, des matériaux utilisés et la façon dont cet art est fait sont d'une immense importance. Je souhaite échanger sur certains de ces principes et méthodes dans mes contributions au Journal des Arts Orthodoxes tout au long des prochains mois, notamment en référence à des icônes, à l'enluminure et aux autres arts du livre. Cela inclura une recherche sur leurs significations symboliques et théologiques, ainsi que leur histoire, les matériaux et les divers aspects techniques.

 Pour commencer, je voudrais explorer le rôle de la matière et du monde matériel dans le culte de l'Église orthodoxe. Ce qui est au cœur de notre compréhension du monde matériel, c'est que la matière est créée par Dieu, qu’elle est bonne, et qu’elle fait partie du plan divin. Cela est exprimé dans Genèse 1:31, «Et Dieu vit toutes les choses qu'il avait faites et voilà, elles étaient très bonnes.» En outre, nous lisons que «Toute grâce excellente et tout don parfait viennent d'en haut, et descendent du Père des lumières». (Jacques, 1:17)

 L'importance de l'expression matérielle du sacré dans le Christianisme Orthodoxe se trouve au centre de notre compréhension de l'Incarnation, comme le dit saint Grégoire de Nysse : «Il a donné à la vie une réalité effective, pour qu'au moyen de la chair revêtue par lui et déifiée avec lui, se trouvât sauvé en même temps ce qui est apparenté à la chair et de même nature.»[2] En outre, lors de la Transfiguration, la grâce est passée de la divinité du Seigneur à sa nature humaine et à ses vêtements qui brillaient. De même, dans l'Église, la grâce du Christ passe, et là, à travers l'humanité qui il partage avec nous et à travers nous cette grâce peut alors passer à tout le monde matériel. Dans Romains 8:21 nous lisons: "... la création elle-même sera affranchie de la servitude de la corruption dans la liberté glorieuse des enfants de Dieu." 

 Comprendre les matériaux de façon plus profonde est absolument essentielle au maintien de l'intégrité et de la beauté des arts liturgiques dans le long terme. L'un des objectifs est de créer des œuvres qui reflètent l'incorruptibilité et la beauté de Dieu et l'utilisation de matériaux pauvres ou inadaptés sape ce symbolisme. Par exemple, la sélection de peintures modernes de fabrication industrielle peut sembler acceptable, mais quand on les examine de près, leurs caractéristiques comprennent souvent des éléments inappropriés ou de qualité médiocre et leurs pigments sont souvent instables à la lumière ou ont été obtenus par des procédés chimiques douteux ou immoraux au cours desquels la couleur résultante est un sous-produit, sans rapport avec l'intention du processus. Quelle comparaison possible avec l’acte de ramasser une pierre unique, la fleur d'une grotte souterraine et le fruit de plusieurs milliers d'années de croissance naturelle? Les couleurs rayonnantes de la malachite ou de l'azurite, par exemple, n'ont pas d'égal dans la palette artificielle et ne s’altèrent pas du tout à la lumière, elles sont durables et ne perdent rien de leur éclat, et sont donc à la fois symboliquement et fonctionnellement particulièrement appropriés pour la réalisation de l'art sacré.

Après que la lumineuse pierre d’Azurite bleue a été broyée et lavée plusieurs fois elle est versée
sur un plat pour sécher et devenir une poudre fine
qui est ensuite utilisée comme pigment pour
l'aquarelle et la peinture tempera à l'œuf.
« Les cieux racontent la gloire de Dieu et le firmament annonce l’œuvre de ses mains ». (Psaume 18:1)

 Sa Sainteté le Patriarche œcuménique Dimitrios a déclaré que "Malheureusement, de nos jours, sous l'influence d'un rationalisme extrême et de l'égocentrisme, l'homme a perdu le sens du sacré de la création ...» [3] Une grande partie de notre compréhension de la symbolique spirituelle inhérente à la matière a été perdue ou corrompue par le point de vue actuel laïque, qui a été façonnée par diverses idéologies non-orthodoxes et sont souvent en contradiction avec la théologie orthodoxe. Une société désacralisée cesse de voir la création en tant que porteur de la sagesse et de l'amour de Dieu, elle la regarde au contraire comme une accumulation de matières premières ayant une valeur économique qui leur est associée. Par exemple, dans le cas de l'or, au lieu de voir l'or comme quelque chose de la source divine et un symbole de la divinité de Dieu, de son amour et de son incorruptibilité, on nous apprend à ne voir que sa valeur monétaire, mais rien de la beauté incandescente de sa substance, rien de son essence intérieure ou de son sens.

 En outre, nos matières premières sont désormais touchées par les effets délétères des procédés industriels et de la pollution: «L'industrie croissante produit de plus en plus des quantités de déchets toxiques dont ne sait quoi faire. L'air, les eaux et le ciel, les éléments qui étaient autrefois purs, prennent aujourd'hui une couleur produite par l’homme.» [4] Les produits d'origine animale tels que l'œuf, qui est utilisé dans la fabrication de la tempera à l'œuf, peuvent être le produit d’un élevage en batterie qui exploite les poules, ce qui compromet à la fois la qualité du matériau et le rôle qui nous a été assigné de prendre soin de la création.

En conséquence de ce qui précède, il est maintenant plus important que jamais que l'artiste liturgique et ceux qui passent des commandes et utilisent les arts liturgiques comprennent et célèbrent l’usage véritable et élevé du monde matériel. Une bonne compréhension de la théologie des matériaux et de notre relation avec eux est au cœur du processus de fabrication et une route vers la compréhension plus profonde du caractère sacré de la création et de la contemplation de la réalité de l'Incarnation.

 Toute la création matérielle dans sa beauté resplendissante est une icône, c'est une image des choses les plus élevées, un cadeau d'amour et de générosité, et un mode de réalisation de la beauté divine. Dans les paroles de saint Jean Chrysostome " La nature est notre meilleur maître. A partir de la création, apprenez à admirer le Seigneur! "

Dessin icône miniature de SainteJeanne la Myrrhoblite
 à l'encre sépia  sur vélin tendu feuille d'or 24 carats
 (fleur et pièce d'un penny pour indiquer la taille). 

 Le culte de l'Eglise orthodoxe concerne la célébration et l'utilisation de tous les aspects de nos sens. Cela inclut la vue, l'ouïe, le toucher, le goût et l'odorat. Il utilise et honore à la fois les matériaux, que ce soit du bois, de l'or ou de la peinture, les matériaux pour l'écriture tels que les encres et les plumes, le pain et le vin sacrés ou la combustion de l'encens parfumé.

 Le but des arts liturgiques, c'est la glorification de Dieu et l'action de grâces. L'humanité, un participant simultanément du matériel et du monde spirituel, a été créée pour rattacher la création à Dieu, afin que le monde puisse être sauvé de la corruption et la mort. Nous avons été créés pour vivre selon un mode eucharistique, par des actions de grâces pour tout ce que nous avons reçu. Par conséquent, ce n'est pas seulement un choix, mais notre responsabilité de faire ce don de remerciement le plus beau peut-être, même si cela signifie parfois un sacrifice supplémentaire et un défi. Une icône durera aussi longtemps que la surface sur laquelle elle a été peinte et les matériaux avec lesquels elle a été faite dureront. Elle est destinée à être un objet tactile liturgique, ce n’est pas seulement une surface peinte, et donc chacun de ses aspects doit être soigneusement pris en compte lors du processus de fabrication. Elle doit être suffisamment robuste pour résister à la pérégrination d'adoration que sera sa vie, tout en restant un véritable et numineux symbole de la beauté de Dieu. 

 Les matériaux utilisés pour créer l'art liturgique n’ont pas seulement leurs caractéristiques physiques habituelles qui peuvent être mesurées par la science, mais aussi un sens profond et un symbolisme qui gouvernent leur emplacement et leur utilisation dans l'environnement sacré. Cela inclut les caractéristiques pratiques et fonctionnelles qui sont un facteur essentiel dans leurs diverses applications. Par exemple, dans la fabrication d'une icône pour un usage extérieur, la pierre, le métal ou même la céramique seraient des choix appropriés, tandis que les icônes textiles ou les icônes dorées ne conviendraient pas. 

 Travailler en harmonie avec la création plutôt que contre elle est d'une grande importance. L'architecture et les arts traditionnels liturgiques emploient souvent des matériaux de construction régionaux s’harmonisant ainsi avec le milieu environnant. Les matériaux naturels sont souvent utilisés dans leurs formes pures et certains matériaux qui sont exceptionnellement rares et précieux, comme le lapis-lazuli, peuvent provenir de terres lointaines en raison de leurs qualités particulières.

 Un morceau de Lapis Lazuli d'Asie centrale, 
le pigment extrait est appelé Lazurite 

L'usage contemplatif de matériaux naturels dans leurs formes pures nous permet également d’apprécier leurs qualités et leur valeur fondamentales.J'ai souvent été frappée en regardant la plupart des anciens manuscrits enluminés que beaucoup des couleurs sont utilisés pures et cela renforce notre capacité à aimer et à apprécier chacune pour ce qui la distingue comme ce qui l’unit aux autres. La malachite, le minium, l'indigo, l’azurite et orpiment sont tous faciles à distinguer comme beaucoup d'autres.

 «Car la grandeur et la beauté des créatures font par analogie contempler leur Auteur (Sagesse de Salomon. 13:5)

 L’aventure de la fabrication d’une œuvre d'art liturgique commence longtemps avant de commencer à construire ou à peindre et ce travail de base comprend également la construction d'une relation personnelle avec des matériaux à un niveau beaucoup plus profond que simplement aller dans un magasin et acheter des articles déjà tout faits sur un comptoir. Pour moi en tant qu'artiste, des progrès dans la technique ont souvent eu lieu après la préparation à la main, avec soin, d'un nouveau matériau et il s’en est suivi que l'expérience de son utilisation s’est ensuite transformée en quelque chose que je n'aurais jamais pu imaginer. L'œuvre terminée est toujours plus belle et rayonnante qu'elle aurait été autrement.


[1] Vêpres de la Nativité
[2] Grande Catéchèse de St Grégoire de Nysse
[3] Discours pour Le jour de La Protection de l'environnement 1er sept. 1989
[4] L'Orthodoxie et la crise écologique Patriarcat oecuménique et WWF (World Wide Fund for Nature International)
 (version française par Maxime le minime d'un extrait d'un article de Christabel Anderson du 10 juillet 2012 paru sur le site Orthodox arts journal
Vous aimerez peut-être: 

SKITE SAINTE FOY - Monastère Orthodoxe en Cévennes
Monastery of Saint Silouan the Athonite in Saint-Mars-de-Locquenay, France LA SAUVEGARDE DE LA CREATION DANS LA TRADITION ORTHODOXE 

Théosis (déification) 

Église orthodoxe Pères, la richesse et le capitalisme
CONVERSATION ENTRE LA MONIALE CORNELIA [REES], ET L’ARCHIMANDRITE GABRIEL [BUNGE] : Nous devons retourner à nos racines.
 

De l'athéisme à l'Orthodoxie en passant par...
Travelers on the Way to the Light
Saint Romain - Abbé du Jura, frère de saint Lupicin (✝ 460)
Monastery of Saint Silouan the Athonite in Saint-Mars-de-Locquenay, France

Jean-Claude Larchet sur différents thèmes de la vie spirituelle en rapport avec Pâques
Orientation Orthodoxe Dogmatique Elaborée
Valaam, l'archipel des moines  

Saint Nil de la Sora: Une Voix dans le Désert

 
Héritage orthodoxe