Εμφάνιση αναρτήσεων με ετικέτα Wanawake wa Afrika. Εμφάνιση όλων των αναρτήσεων
Εμφάνιση αναρτήσεων με ετικέτα Wanawake wa Afrika. Εμφάνιση όλων των αναρτήσεων

Παρασκευή 23 Ιουνίου 2017

Ndoa, Mitara na Kanisa la Orthodox


 
Ndoa ya Waorthodoksi Tanzania (kutoka hapa)

Sw.wikipedia
 
Kiongozi wa kabila la Toba 
na wake zake, 1892.
Mitara (au Upoli au Upali) ni hali ya watu zaidi ya wawili kuishi katika uhusiano wa kindoa.
Hali hiyo ilikuwa ya kawaida barani Afrika, ambapo mwanamume mmoja aliweza kuwa na wanawake zaidi ya mmoja, lakini kwa sasa inazidi kupungua.
Ya nadra zaidi ni hali ya wanaume kadhaa kuchanga mwanamke mmoja.
Baadhi ya nchi zinakubali hali hiyo, lakini nyingi zinaikataza.
Vilevile baadhi ya dini zinakubali mitara, hususan Uislamu, lakini nyingine zinaikataza, hususan Ukristo.
Katika Biblia tunakuta maendeleo ya ufunuo kuhusu hali hiyo kati ya Agano la Kale na Agano Jipya. 

Marejeo hapa.

Ndoa ya Wakristo ("kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa")

Sw.wikipedia / Ndoa (sakramenti)
 
“Siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwepo. Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake” (Picha kutoka hapa)

Ndoa kati ya wabatizwa wawili inahesabiwa na Kanisa Katoliki na Waorthodoksi kama mojawapo kati ya sakramenti saba zilizowekwa na Yesu Kristo.


Pamoja na Daraja takatifu ni kati ya sakramenti mbili za kuhudumia ushirika.

Fumbo la ndoa

Kadiri ya mpango wa Muumba, ndoa halisi ina sifa tatu: umoja, uimara na utayari wa kuzaa. “Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke, akasema, ‘Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja?’ Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe” (Injili ya Mathayo 19:4-6). “Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, ‘Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha’” (Mwanzo 1:28). Mitara, uzinifu, talaka, ushoga na kukataa uzazi ni kinyume cha mpango huo.
Muungano usiovunjika mpaka kufa kati ya mwanamume mmoja na mwanamke mmoja waliobatizwa, ambao unafanyika kwa makubaliano yao ya hiari ambayo yanathibitishwa na Mungu anayewatia neema zinazohitajika waweze kutimiza malengo ya ndoa, ni ishara ya muungano wa kiarusi wa Yesu na Kanisa.
Yesu aliweka sakramenti ya ndoa kwa sababu ya umuhimu wa familia kwa ustawi wa mume na mke, watoto, jamii na ufalme wa Mungu, na kwa sababu ya uzito wa majukumu yanayohusika. “Siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwepo. Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake” (Injili ya Yohane 2:1-2), akaleta divai bora ya ndoa sakramenti badala ya ndoa ya kimaumbile. Hivyo ametuandalia neema tuweze kushinda “ugumu wa mioyo” (Mathayo 19:8) unaohatarisha daima uzuri wa mpango wa Mungu kuhusu upendo mwaminifu katika ndoa. “Mungu aliona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana” (Mwanzo 1:31).




Ndoa ya Waorthodoksi Bujumbura (kutoka hapa)

Adhimisho la sakramenti ya ndoa

Ndoa ya Wakristo ni sakramenti ya Yesu na Kanisa lake. “Njoo huku, nami nitakuonyesha yule Bibi arusi, mke wa Mwanakondoo” (Ufu 21:9). Wakiwa na ndoa halisi, mume na mke waliobatizwa ni ishara wazi ya hao wanaarusi wawili wasioonekana. “Kama vile Kanisa limtiivyo Kristo, vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo. Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake” (Ef 5:24-25). Ndiyo sababu Mkatoliki hawezi kufunga ndoa bila ya kuhusisha Kanisa na kufuata taratibu zake.
Kwa kawaida Wakatoliki wanaiadhimisha wakati wa Misa, karamu ya arusi ya Mwanakondoo na Kanisa, lakini wanakubali katika mazingira ya pekee iweze kufungwa na wanaarusi mbele ya mashahidi wawili hata bila ya kuwepo padri .
Kumbe Waorthodoksi wanahesabu baraka ya padri kuwa sehemu ya lazima ya sakramenti, ambayo wanaarusi wanapewa.

Kubariki ndoa kwa Waprotestanti

Martin Luther aliona sakramenti sharti iwe alama iliyowekwa na Yesu Kristo mwenyewe, lakini ndoa ni sehemu ya utaratibu wa uumbaji uliotangulia kuja kwa Yesu.
Kwa sababu hiyohiyo Waprotestanti wengi hawakubali ndoa kuwa sakramenti na wanabariki tu ndoa iliyofungwa kufuatana na sheria za dola.


Ndoa ya Waorthodoksi Madagascar (kutoka hapa)
 
Tunaelewa kuwa mtu wa Kiafrika na wake wengi anaweza kuwapenda wote. Tunaheshimu hii. Lakini katika Agano la Kale, Mungu aliumba jozi la kwanza la watu, mtu mmoja na mwanamke mmoja tu, Adamu na Hawa. Hii inathibitisha kwamba mwanamume na mwanamke ni wa thamani sawa. Pia inathibitisha kuwa ndoa pekee ambayo Mungu anapenda kweli, ni ndoa kati ya mtu mmoja na mwanamke mmoja.
Kwa hiyo, katika Kanisa la Orthodox, ambalo anakupenda mwanadamu (mwanamume na mwanamke) sana, mitara haiwezi kukubalika.




Bibi na arusi wakati wa harusi Waorthodoksi (hapa)
Ona pia

Polygamy in Africa and Orthodox Church
Orthodox Women Saints (picha)
Orthodoxes chrétiens Mariages en Afrique 
Which One Should I Deny? / "Leave, you who loves him more..." - A True Story from the Years of the Missionary Fr. Cosmas Grigoriatis
Theotokos

Wanawake wa Afrika 
Femmes Africaines

African Women

Male and Female Created He Them  
Wakristo Orthodox ya Afrika 
Kanisa la Orthodox na Kanisa Katoliki  
KUTAFUTA IMANI LAKUNYOLOKA – AMA KI ORTHODOKSI  

 Ndoa ya Waorthodoksi Pwani ya Pembe (kutoka hapa - video hapa)

Κυριακή 25 Οκτωβρίου 2015

MWANAMKE NI MAMA WA DUNIA


African Brotherhood Foundation
 
Picha hapa
African Brotherhood Foundation (ABF) ni taasisi changa yenye malengo na nia thabiti ya kuwaunganisha waafrika wote katika nyanja zote za kijamii, kiuchumi na kisiasa. Hivyo basi tunaamini kiu kubwa ya waafrika ni kuona Afrika inaungana, sisi tumeamua kulisimamia suala hili ili kutimiza ndoto za waasisi wa umoja wa Afrika ambao nyuma yao walikuwepo wanawake katika mapambano ya kutafuta uhuru wa bara la Afrika.
Mtazamo wa African Brotherhood Foundation, kama ilivyo siku zote katika dunia, mungu ameumba vitu mbalimbali kwa maana yake. Leo hii kona ya ABF Africa imeona igusie na kuelezea juu ya mwanamke. Kimantiki ndani ya dunia hakuna mwanadamu asiye zaliwa na mwanamke na watu wote ni lazima tuwathamini wanawake. Sifa za mwanamke katu hatuwezi kuzimaliza kwa maana thamani yake ni kubwa na zenye kuvutia ukizisikiliza na kuziona. Katika bara letu la Afrika wanawake wana mchango mkubwa sana. Busara zao ndizo zilichangia Afrika kuwa huru mpaka hivi sasa ingawa wadai uhuru wa nchi nyingi za Afrika walikuwa ni wanaume. Lakini ukitazama utaona mwanamke alikuwa nyuma ya mwanaume kwa kumpa mawazo na muelekeo mzuri ndio maana mambo yalikwenda kwa kasi na uweledi kwasababu kama tunavyo jua mwanamke akilala jamii imelala.
Hebu tazama mwanamke alivyokuwa mbunifu. Familia nyingi za bara hili la afrika zinategemea uwepo wa mwanamke ili ziweze kupata maendeleo ya mali, chakula na hata mavazi. Hii ni kwa sababu yeye ndiye chanzo cha ufanisi katika jamii kwenye kutimiza wajibu wa kila siku. Mungu aliwaumba kwa makusudio maalumu ya kuisaidia na kuikomboa jamii sio kuwa wasindikizaji kama madai ya baadhi ya watu wenye fikra potofu na mawazo mgando. Kona ya ABF Africa inapenda kuwaambia watu wanaonyanyasa wanawake waache mara moja, hivi nyie hamna huruma wala chembe ya ubinadamu hata kidogo? Mama amebeba ujazito wako miezi tisa, amejifungua kwa uchungu na kukulea kwa shida na dhiki na kufikia kipindi chakula nyumbani hakuna aliweza kutumia maarifa ya ziada kwa kuchemsha mawe ili akupe moyo na kutuliza njaa yako? Vilevile kufanya jitihada kwa kupata chakula kwa siku inayo fuata iwe kwa kukopa au njia nyingine lakini leo hii wewe binadamu usiye na huruma wala shukurani kwa mwanamke unamdharau na kumnyanyasa! Tambua amani unayo iona hii imetokana na yeye kwa sababu ndiye chanzo cha amani duniani kwa ujumla kutokana analeta utulivu na kuzuia jazba za kina baba majumbani. Leo sisi ni mashuhuda viongozi wengi wanapendeza na kupanda majukwaani na kujinasibu ni kazi kubwa inayofanywa na wanawake kwa utashi mkubwa waliopewa na mungu.
Asiye mpenda mwanamke asipewe kipaumbele cha aina yeyote ile katika jamii, ushujaa wa mwanamke upo kwenye mafungu yote ya kinadharia na kivitendo. Mtazamo wa kona ya ABF Afrika ni kuona Afrika inaungana ili kukata kiu kubwa ya watu wengi wa bara letu. Hii ndio maana imeamua kumuelezea mwanamke kwa kutambua kabisa bila ya yeye kuwepo na kushirikishwa muungano tunao upigania hauwezi kupatikana bila michango yao. Na kwa kulifahamu hilo ni lazima tuwashirikishe moja kwa moja na kuungana nao kwenye harakati zao zote za mabadiliko kimaneno na vitendo.

 
Maasai Maasai, Kenya (hapa na hapa)

Jamii za kiafrika zinapaswa zibadilike ili ziweze kupata maendeleo vilevile zitambue kwenye kila jambo la kimaendeleo kuna mwanamke, kona ya ABF Afrika itaendelea kulaani mateso, ukandamizaji, ukatili na unyanyasaji dhidi ya mwanamke bila ya kificho wala uwoga wa aina yeyote. Kama taasisi changa ya AFRICAN BROTHERHOOD FOUNDATION (ABF) kwa pamoja tunatambua mchango mkubwa unaofanywa na mwanamke, huu sio wakati wa kulalamika, mtumie fursa za kujenga hoja zenye mantiki na zenye kuleta mabadiliko kwenye jamii za kiafrika. Kwa maana hiyo kushirikiana na mwanamke kutaleta misingi ya uzalendo, utawala bora, umoja na mshikamano wa hali ya juu kwa bara la Afrika.
Vilevile tunatambua michango iliyofanywa na inayofanywa na wanawake katika bara hili shukrani kubwa kwa marehemu Bibi TITI MOHAMED, Mama MARIA NYERERE, Mama GRACE MACHEL, Mama WINNIE MADIKIZZELA MANDELA , Mama SALMA KIKWETE, HELLEN SELIF JOHNSON, DKT. ASHA ROSE MIGIRO, PROF ANNA TIBAIJUKA na wengine wote kwa michango yao iliyotupelekea tupate uhuru na maendeleo ya bara la afrika. Wanawake wote hawapaswi kukata tamaa, wanapaswa kuongeza juhudi na kuunganisha maarifa yao kwa pamoja wataleta maendeleo endelevu na kulifanya bara la afrika kwenda mbele.
Wito wetu kwenu ni kuwaasa mtumie nafasi mnazo zipata kudumisha umoja wenu pamoja na ule wa Afrika, tusisubiri maadhimisho ya kila mwaka bali tushirikiane pamoja kila wakati na kupambana na wale wote wasio watakia mema. Ni vyema kupambana nao kwa sheria ili iweze kuwa fundisho kwa wale wanao wanyanyasa wanawake na kuwanyima haki zao za msingi. Kuliko kuwaacha na kuzidi kuwafanyia wanawake matendo maovu yasio stahili katika jamii na kuzidi kuwarudisha nyuma.
Vilevile kwa upande wa serikali za Afrika zitazame kwa umakini sekta ya afya hususani kwa upande wa wodi za wazazi. Hospitali nyingi hazina vifaa vya kutosha ukiangalia kitanda kimoja utakuta watu zaidi ya mmoja hii ina hatarisha afya ya mama na mtoto hebu tuwe na chembe ya huruma kwa hawa mama zetu, bila ya wao tusinge kuwa hapa tulipo na jamii yeyote bila ya mwanamke haiwezi kuendelea.
Serikali ina wajibu wa kutunga sheria itakayo mlinda mwanamke na kumpa utambulisho katika jamii kutokana mila potofu zimekuwa zikimnyima haki za kimsingi kama vile kuzuiliwa kwenda shule, kutokuwa na maamuzi katika jamii. Hivyo basi ili kumsaidia mwanamke kuondokana na manyanyaso anayoyapata kila siku hakuna asiyejua kama mwanamke anaweza kufanya mabadiliko yaletayo tija na manufaa kwa jamii zetu tumeweza kuona baadhi yao na tuna mifano ya kuwazungumzia na kujivunia uwepo wao.


Christina Mothapo with members of her family on her 87th birthday, 1 Jan 2013 
Christina Mothapo, Mamelodi (hapa)

Kuna umuhimu mkubwa wa kutungwa kwa sera ya kumlinda na kumtetea mwanamke. Ni jukumu la serikali na wadau kwa kushirikiana kwa pamoja. Hii itamuwezesha mwanamke kutoka kifungoni alipo kwa muda mrefu sasa bila ya hatia yeyote, hivi ni kosa kwa wao kuwepo duniani? Au wemepoteza uhalali wa kuishi? Maana tafsiri potofu za baadhi ya watu zimewafanya wanawake kuwa kama yatima waliokosa misaada ya kimaisha. AFRICAN BROTHERHOOD FOUNDATION (ABF) imeona “ni bora kufa kuliko kuishi na hisia zilizo kufa” kwa kulikemea hili kwa nguvu moja na kutangaza rasmi uadui na wale wote wanaomtesa na kumnyanyasa mwanamke na kuzitaka jamii zote za Afrika kushirikiana katika kumkomboa mwanake kwa nguvu moja.
Mwisho, wakati wa kusimamisha haki za wanawake umefika. Afrika ni mali ya watu wote. kuheshimiana na kuvumiliana itajenga jamii ya watu wenye fikra hai zenye mashiko ndipo maendeleo yatapatikana bila ya kupiga hodi wala foleni kwa kusubiri misaada kutoka ughaibuni. Mwanamke ndiye nguzo na mustakabali wa bara la Afrika na dunia kiujumla.


Ona pia

Bikira Maria, Mama wa Mungu
African Women 
Mother of God (Virgin Mary), Orthodox Church and African peoples

Ethiopian Slave Girl Beaten By Saudi Family ?

Παρασκευή 16 Οκτωβρίου 2015

Wasi wasi wa UNICEF kuhusiana na hali ya watoto wakimbizi wa Nigeria


Iran Swahili Radio, Alkhamisi, 30 Julai 2015

Wasi wasi wa UNICEF kuhusiana na hali ya watoto wakimbizi wa Nigeria


Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa UNICEF umeelezea wasi wasi mkubwa ulionao kutokana na kuendelea vitendo vya utumiaji mabavu vya kundi la Boko Haram ambavyo vimepelekea mamia ya maelfu ya watoto nchini Nigeria kuwa wakimbizi. Ripoti ya UNICEF iliyotolewa Jumanne ya jana imeeleza kuwa, mashambulio na vitendo vya utumiaji mabavu vya Boko Haram katika miaka ya hivi karibuni vimepelekea watoto zaidi ya laki nane wa Nigeria kuwa wakimbizi. Ripoti hiyo inasema, akthari ya watoto hao wamelazimishwa kuolewa au wamebakwa. 
Takwimu za hivi karibuni za Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa zinaonesha kuwa, katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita idadi ya watoto ambao ni wakimbizi nchini Nigeria imeongezeka maradufu.  Wakimbizi wa Kinigeria wamekuwa wakikimbilia katika nchi za Chad, Cameroon na Niger ambazo zenyewe ni miongoni mwa nchi masikini duniani na hivyo kutokuwa na uwezo wa kuwalinda au kutoa huduma muhimu kwa wakimbizi hao. Ripoti zinaonesha kuwa, hata wanawake na watoto walioko katika kambi na vituo vya kimataifa vya Umoja wa Mataifa katika maeneo ya mpakani hawako salama. 
Tangu kundi la Boko Haram lianzishe mashambulio yake nchini Nigeria hadi sasa zaidi ya raia milioni mbili wamelazimika kuyaacha makazi yao na kuwa wakimbizi. Wataalamu wa mambo wanasema kuwa, jinai dhidi ya wanawake na watoto nchini Nigeria na katika nchi jirani na nchi hiyo ambazo zinashuhudia harakati za Boko Haram zimekuwa zikiendelea kufanyika. Siku chache zilizopita Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa UNICEF ulitangaza kuwa, kwa akali asilimia 75 ya mashambulio ya kujitolea muhanga yaliyotekelezwa nchini Nigeria mwaka huu yamefanywa na wanawake na watoto. Kwa mujibu wa takwimu za shirika hilo ni kuwa, katika miezi mitano ya awali ya mwaka huu, takribani mashambulio 27 ya kujilipua yalifanyika nchini Nigeria huku 9 kati ya hayo yakiwa yametekelezwa na watoto wenye umri wa kati ya miaka 7 na 17. Wanawake na watoto hao wamekuwa wakitekeleza mashambulio hayo ya kujilipua baada ya kupikwa kifikra na wanamgambo wa Boko Haram wakati wakishikiliwa mateka.
Hata kama Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameelezea kusikitishwa kwake katika taarifa mbalimbali alizotoa kuhusiana na kupanuka wigo wa mashambulio ya Boko Haram katika nchi za Kiafrika, kuongezeka utekaji nyara watu, kubakwa wanawake na mabinti na kutumiwa watoto kama mabomu ya watu, lakini pamoja na hayo hakuna hatua yoyote ya maana iliyochukuliwa na Umoja wa Matifa kwa ajili ya kukabiliana na hali hiyo mbaya. Wachambuzi wa mambo wanaamini kuwa, baada ya kuingia madarakani Rais Muhammadu Buhari nchini Nigeria kulijitokeza matumaini ya kuokolewa nchi hiyo na raia wake kutoka mikononi mwa jinamizi la mashambulio ya kundi la kigaidi la Boko Haram, lakini baada ya kupita miezi miwili tangu aingie madarakani kiongozi huyo, wimbi la mashambulio ya Boko Haram limeshadidi na inaonekana kuwa, viongozi wa kimataifa ambao walipaswa kumsaidia Buhari na waitifaki wake katika kupambana na kundi hilo la kigaidi na kurejesha utulivu nchini Nigeria, hawana msaada mwingine ghairi ya kuonyesha masikitiko yao tu kuhusiana na hali hiyo.

Τρίτη 4 Αυγούστου 2015

Habari Kutokanyumba la Watawa Mukanisa la Orthodoksi Mtakatifu Nektario Mudji wa Kolwezi Inchi la Kongo Baada Zaire



Nyumba la watawa katika kanisa la Mtakatifu Nektario

KUTWAA KIPAWA LA KITAWA KWA BINTI
 

Diakonima

Katika inchi la Kongo na Mudji Kolwezi kuna Mama mtawa wa kwanza jina lake Thekla,anakaa kukanisa la Mtakatifu NEKTARIO, naye ni mtawa wa kwanza katika Afrika mzima tokeya mwaka 1988. Mpaka leo alikuwa na watawa ine,kwa mapendo ya Mwenyezi mtawa wa tano anaongezeka mu mwezi wa saba 2009 Hivi kipawa la kitawa kilitwala kwa Mwaskofu wa Katanga Mweshimiwa Meletio.



Mama mtawa mkubwa Thekla na mwana funzi binti mbele ya kuwa mtawa

Mtawa wa sasa alipata jina la AGNIESE, ni mtoto wa padiri,ana na miaka 24, Alikuwa najifunza kunapita miaka tano karibu na wa tawa wengine kanisani.



Kutwaa kipawa la kitawa la Agniese ku mkono la Askofu Mweshimiwa Meletio

Hizi habari za kupasha Neno la Ukweli katika Kiorthodoksi ni mambo Ya MIUJIZA katika myoyo yawa ndugu wenye AFRIKA CHINI LA SAHARA.



Kiisha kutwaa kipawa la kitawa, mtawa Agniese na Askofu

Ni furaha katika Bwana kwakuwona Ngufu la Roho Mtakatifu na kutumikisha wa tumishi wa Bwana hama Mwaskofu Katanga Mweshimiwa Meletio mtoka mlima takatifu la Athosi mu Monastari Grigoriou, yeye alimpiana marehemu padiri Kosma, Mpaka leo anaendelesha na kupasha NENO LA UKWELI, na kubatiza ma elfu ya wa pagani,na kujenga makanisa pamoja na ma nyumba la wa padiri ,tena anajenga ma masomo,kwanza primari,sekundari,masomo la kazi na lamikono,wanafunzi wanakuja ma elfu,walimu wengi,ivi tunamwomba Bwana asaidiye kazi lake liendeleye na watumishi wa haki wakudje shambani lake watumike.



Mtawa wasasa, ivi machoni mwake anaagaa na mwangaza la neema.

Mwenyezi apate kumu saidiya achunge hii baraka kila siku la maisha lake.

Tazama hapa


KUTAFUTA IMANI LAKUNYOLOKA – AMA KI ORTHODOKSI

Umonaki katika Kanisa la Orthodox 

Wamisionari tano halisi ambaye heri Afrika kusini mwa Sahara
(na takatifu mtoto bila majina ya Afrika)


The historical background of the monastery in Kolwezi, Congo (DRC)
Orthodox Mission in Tropical Africa (& the Decolonization of Africa)
Liturghia Takatifu